Nafasi za Kuandikishwa Jeshini – JWTZ – May 2025
1.Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linatangaza nafasi za kuandikishwa Jeshini kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu kuanzia elimu ya Sekondari hadi elimu ya Juu. Aidha, uandikishaji utahusisha vijana wa Kitanzania wenye Taaluma Adimu.
2.Wataalamu hao watakaoandikishwa Jeshini watapatiwa mafunzo mbalimbali muhimu ya Kijeshi na mafunzo ya kuwaendeleza katika taaluma zao.
SIFA ZA MWOMBAJI
3.Vijana wa Kitanzania wenye nia ya kuandikishwa Jeshi wanatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-
a. Awe raia wa Tanzania mwenye kitambulisho cha Taifa. b Awe na afya nzuri na akili timamu,
c.Mwenye tabia na nidhamu nzuri, hajapatikana na hatia ya makosa ya jinai mahakamani na kufungwa.
d.Awe na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate), vyeti vya Shule na vyeti vya Taaluma.
e.Awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi cha Kuzuia Magendo.
f.Awe amehitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mkataba wa kujitolea au Mujibu wa Sheria na kutunukiwa cheti.
g.Kwa vijana wenye elimu ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita wawe na umri usiozidi miaka 24, Vijana wenye elimu ya Stashahada umri usiozidi miaka 26, Vijana wenye elimu ya Juu umri usiozidi miaka 27 na Madaktari Bingwa wa Binadamu umri usiozidi miaka 35 ya kuzaliwa.
4.Taaluma Adimu zinazohitajika ni ifuatavyo:-
a. Taaluma ya Tiba
(1) Medical Doctor (Specialist)
Generall Surgeon, Orthopaedic Surgeon, Urologist Radiologist, ENT Specialist, Anaesthesiologist, Physician,
Ophthalmologist, Paediatrician, Obstetrician & Gynaecologist, Ocologist, Pathologist, Psychiatrist, Emergency Medicine Specialist na Haematologist.
(2) Medical Doctor, Dental Doctor, Veterinary Medicine, Bio Medical Engineer, Dental Laboratory Technician, Anaesthetic, Radiographer, Optometry, Physiotherapy na Aviation Doctor.
b.Taaluma za Uhandisi (Engineer).
Bachelor of Electronic Engineering, Bachelor of Mechanical Engineering, Bachelor in Marine Engineering, Bachelor in
Merine transportation and Nautical Science, Bachelor in Mechanics in Merine Diesel Engine, Bachelor in Aviation Management, Bachelor in Aircraft Accident and Incident Investigation, Bachelor in Meteorology, Air Traffic Management na Aeronautic Engineering.
c.Fundi Mchundo.
Aluminium Welding na Welding and Metal Fabrication.
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI KWA MAKUNDI YOTE MAWILI
5. Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yawasilishwe Makao
Makuu ya Jeshi Dodoma kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 hadi tarahe 14 Mei, 2025 yakiwa na viambatisho vifuatavyo:-
a.Nakala ya Kitambulisho cha Taifa au nambari ya NIDA.
b.Nakala ya cheti cha kuzaliwa, vyeti vya Shule na Chuo.
c.Nakala ya cheti cha JKT kwa waombaji waliomaliza mkataba wa kujitolea.
d.Nambari ya simu ya mkononi ya mwombaji.
MAOMBI YATUMWE KWA ANUANI IFUATAYO
Mkuu wa Utumishi Jeshini,
Makao Makuu ya Jeshi,
Sanduku la Posta 194,
DODOMA, Tanzania
Soma Pia: Tangazo la Kazi: Nafasi za Udereva – School of St Jude